Dar
es Salaam. Wapinzani wa Yanga timu ya Komorozine de Domoni kutoka
Comoro watatua nchini leo tayari kwa mchezo wa Jumamosi wa Ligi ya
Mabingwa Afrika utakaopigwa Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa.
Yanga
imepangwa kuanza na Wacomoro hao katika hatua ya awali ya mashindano
hayo makubwa ya klabu barani Afrika. Wakifanikiwa kusonga mbele
watavaana na Al Ahly ya Misri. Mchezo huo wa Yanga utachezeshwa na
waamuzi kutoka Somalia wakati wenzao wa Azam watachezeshwa na waamuzi
kutoka Sudan Jumapili ijayo. Ofisa habari wa Yanga, Baraka Kizuguto
alisema jana kikosi chao kipo Bagamoyo kujiandaa na mchezo huo.
“Bagamoyo ndiyo kambi yetu ya kudumu hadi Ligi na mashindano yote
tumalize. Kila kitu kinaenda vizuri, wachezaji wanaanza mazoezi rasmi ya
kuwakabili Wakomoro leo (jana), baada ya mapumziko ya siku moja.”
alisema
Hata hivyo Yanga itashuka dimbani bila ya mchezaji wao tegemeo Emmanuel
Okwi ambaye amezuia kucheza na Kamati ya Maadili na Hadhi ya Wachezaji
baada ya usajili wake kuwa na utata na kusubiri ufafanuzi kutoka
Shirikisho la Soka duniani (FIFA).
Akizungumzia suala la mshambuliaji huyo Bonifance Wambura alisema “Fifa
tulishawakumbusha kuhusu ufafanuzi tulioomba wa Okwi, wametujibu kuwa
wameshapata barua yetu na wataifanyia kazi, ni lini sijui, ndiyo
tunasubiri mpaka watakapotujibu.” alisema
Azam nao wameingia kambini jana kujiandaa na mchezo wao dhidi ya
Ferroviario De Beira ya Msumbiji katika raundi ya awali ya Kombe la
Shirikisho.
Iwapo timu hiyo yenye maskani yake Chamazi itafanikiwa kuwanyuka
Ferroviario na kuvuka hatua hiyo watamenyana na mshindi kati ya St
Michel ya Shelisheli na ASSM Elgeco Plus ya Madagascar.
Mwananchi
No comments:
Post a Comment
Toa maoni yako lakini angalia kuchafua hali ya hewa na usimuumize mwenzako