A

A

RATIBA YA MATEMBEZI YA HIYARI KWAMIGUU DAR MPAKA MORO YAKAMILIKA

001Mwenyekiti wa Kamati ya Vijana Wapenda Amani Tanzania, Said Mwaipopo (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya habari (MAELEZO), jijini Dar es Salaam Januariy 8-2014,kupinga mapendekezo ya rasimu ya Katiba mpya kuwepo kwa serikali tatu. Kushoto ni Katibu wa kamati hiyo, Chifu Msopa.
PICHA NA PHILEMON SOLOMON  WA  FULLSHANGWE  DAR  ES  SALAAM
…………………………………………………………………..
Kuanzia tarehe 11.01.2014 Matembezi ya hiyari kwa miguu kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro yataanza rasmi yakikadiriwa kuchukua siku zisizozidi kumi, lengo kuu likiwa ni kuhamasisha, kukumbushana na kuenzi Umoja, Amani na Utulivu kama Taifa moja likaitwa Tanzania ilhali juhudi yakinifu kuanzia ngazi ya mwananchi mmoja mmoja, familia, kaya, wilaya mpaka Taifa kujivika jukumu la kufahamu, kupambanua, kudadavua na mwisho wa siku kushirikiana kupitia njia za makusudi kuhakikisha maliasili na utajiri wa Taifa hili jadidu unamnufaisha kila Mtanzania, huku masuala ya Elimu, Afya, Ustawi wa Jamii, Ujasiriamali na Taaluma yakitiliwa mkazo pasi kuachwa kando.
Matembezi haya yanatarajiwa kuwa na vituo kadhaa vikiwemo ; Kibaha, Mlandizi, Vigwaza, Chalinze, Mikese na kumalizia Morogoro, tunatarajia ndugu zetu Watanzania tujikimu kwa mahitaji kadha wa kadha tuwapo safarini, Nchi ikiwa Yetu, Wajibu ukiwa Wetu na UTAIFA tukiuweka na kuutanguliza mbele.
Mpaka sasa matembezi haya ya hiyari yenye kauli mbiu Nchi Yangu, Wajibu Wangu : UTAIFA KWANZA hayajapata mdhamini yeyote na maandalizi yote mpaka sasa ni kufikia lengo la matembezi kama Tanzania iliyo moja bila kujali itikadi, imani, dini, asili ama hata tofauti za kiuchumi miongoni mwetu na kuangaza katika Tanzania yenye kutoa nafasi kwa kila Mtanzania.
Kwa hakika maandalizi ya msingi yamekamilika na tarehe 11.01.2014 ndoto yetu ya kufanya matembezi ya hiyari yatafikisha ujumbe ulio wa Amani na Ustawi wa Taifa letu itachukua nafasi na kuwa halisia.
Nchi Yangu, Wajibu Wangu : UTAIFA KWANZA

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako lakini angalia kuchafua hali ya hewa na usimuumize mwenzako