Taarifa iliyotolewa na Afisa habari wa Umoja huo, Susanne Mbise,
ilisema kesho, mkuu wa EU nchini, Balozi Filiberto Sebregondi na
mratibu wa UN pamoja na mwakilishi wa UNDP nchini, Alberic Kacou
watasaini na kuzindua rasmi ushirikiano wa EU-UNDP.
“Katika msaada huo wa kusaini kwenye uchaguzi wa Tanzania, Programu
ya Uwezeshaji Demokrasia (DEP), shughuli hiyo itahudhuria na mwenyekiti
wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva,”
ilisema taarifa hiyo.
Taarifa hiyo iliongeza kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha pamoja na wanachama wa kamati ya
taifa ya Uendeshaji ya DEP na wawakilishi wa taasisi maalum za uchaguzi
watashuhudia hafla hiyo.
“Wengine watakaokuwepo kesho katika ofisi zetu za EU ni mashirika
ya kiraia yanayoshiriki katika uchunguzi wa ndani, usimamizi wa upigaji
kura na elimu ya uraia,” ilisema.
Tanzania itafanya uchaguzi wake mkuu wa madiwani, wabunge na Rais
mwaka ujao, mara baada ya kupatikana kwa Katiba Mpya ambayo huenda
ikaruhusu uwepo wa serikali tatu, Tanganyika, Zanzibar na Muungano wa
Jamhuri ya Tanzania.
CHANZO:
NIPASHE JUMAPILI