Mke
 wa Rais Mama Salma Kikwete akihutubia mkutano wa Mawaziri kutoka nchi 
za Mashariki na Kusini mwa Afrika kuhusu elimu ya afya ya uzazi kwa 
vijana wa nchi hizo. Mkutano huo wa siku mbili unafanyika nchini Afrika 
Kusini katika Mji wa Cape Townleo.
 Mke
 wa Rais Mama Salma Kikwete akitoka kwenye ukumbi wa mkutano baada ya 
kuufunga rasmi huku akisindikizwa na washiriki baada ya kutoa hotuba 
(BEYOND THE COMMITMENT) iliyosisimua wajumbe wa mkutano huo.
 Mawaziri
 wa Elimu na Afya kutoka nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika wakiapa 
kwa niaba ya nchi zao kutekeleza majukumu waliyopitisha kwenye kikao cha
 High Level Group, kuhusiana na elimu ya afya ya uzazi ( comprehensive 
sexuality education and sexual and reproductive health services) 
mwishoni mwa kikao cha siku mbili kilichofanyika huko Cape Town.
 Mke
 wa Rais Mama Salma Kikwete akipiga picha na Mkurugenzi Mtendaji wa 
UNAIDS, Bwana Michel Sidibe wakionyesha umuhimu wa dhana nzima ya 
mkutano wa High Level Group ( YOUNG PEOPLE TODAY, TIME TO ACT NOW) 
kuhusiana na masuala ya elimu ya afya ya uzazi kwa vjijana katika nchi 
za Mashariki na Kusini mwa Afrika.
 Mke
 wa Rais Mama Salma Kikwete akipongezwa na Dr. Julitha Onabanjo, Naibu 
Mkurugenzi Mkuu wa UNFPA kwa hotuba aliyoitoa wakati wa kufunga mkutano 
wa siku mbili wa Mawaziri wa Elimu na Afya kutoka katika Nchi za 
Mashariki na Kusini  mwa Afrika huko Cape Town.
  Baadhi
 ya washiriki wa mkutano waqkisikiliza hotuba ya ufungaji iliyokuwa 
ikitolewa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete huko Cape Town nchini Afrika
 Kusini.
Mke
 wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa pamoja na viongozi waandamizi 
waliohudhuria mkutano wa High Level Group hukom Cape Town wakisimama kwa
 dakika moja kwa ajili ya kumkumbuka hayati Rais Nelson Mandela. Kutoka 
kushoto ni Bwana Enver Surty, Waziri wa Elimu ya Msingi wa Afrika 
Kusini, Dr. Festus Mogae, Rais Mstaafu wa Botswana, Mama Salma, Bwana 
Luiz Loures, Naibu Mkurugenzi Mtendaji, UNAIDS, Dr. Julitha Onabanjo, 
Naibu Mkurugenzi Mkuu, UNFPA, Bwana Qian Tang, Naibu Mkurugenzi 
Mkuu-Elimu- UNESCO, Bwana Geeta Rao Gupta, Naibu Mkurugenzi Mtendaji, 
UNICEF. Picha zote na John Lukuwi
No comments:
Post a Comment
Toa maoni yako lakini angalia kuchafua hali ya hewa na usimuumize mwenzako