A

A

Wema Sepetu ndani ya “Kwachukwachu” ya Martin Kadinda.



c5526dfabd2311e3afd612c1253656db_8
Baada ya kufanikiwa sana kwa mavazi yake yaliyojulikana “Single Buttons”, sasa mbunifu maarufu wa mavazi hapa nchini Martin Kadinda katambulisha aina mpya ya mavazi yajulikanayo kama  ”Kwachukwachu”. Aina hii mpya ya mavazi imepokelewa vizuri sana kwani siku chache  tu baada baada ya kutambulisha mavazi hayo Diamond Platnumz aliamua kumuunga mkono kwa kununua shati la “Kwachukwachu”. Diamond alionekana amevaa shati hilo katika video iliyowahusisha wasanii wakubwa 19 kutoka Afrika.
Siku ya leo kupitia akaunti yake ya Instagram, Martin Kadinda katambulisha mavazi ya Kwachukwachu ambayo yatakua yakivaliwa na wadada. Martin aliweka picha za Wema akiwa kavaa Gauni fupi la Kwachukwachu.