STRAIKA
wa Mgambo, Mohammed Neto ambaye aliondolewa uwanjani kwa kupewa kadi
nyekundu katika mechi dhidi ya Yanga, amefunguka kuwa hata kama alikuwa
amebeba hirizi, atakuwa amefanya hivyo kwa faida yake huku akisema mbona
wachezaji wengine wakibeba hawaandikwi kwenye magazeti!
Neto ambaye katika ripoti ya mwamuzi wa mechi hiyo, Alex Mahagi na
kamisaa wa mchezo, Tito Haule, iliripotiwa kuwa alitolewa kutokana na
kuwa na bisibisi, amewaka kwa kusema hakuwa na bisibisi wala hirizi
lakini kama ni hirizi kuna wachezaji kama kina Mrisho Ngassa wa Yanga
wanabeba kwenye mechi na hawalalamikiwi.
Mshambuliaji huyo mwenye mwili mkubwa, amelalama kuwa yeye hakuwa na
silaha yoyote, hivyo anashangaa taarifa kuwa alikuwa amefunga hirizi
sehemu za siri.
“Mi nashangaa sana nyie watu wa magazeti mnaniandika nimebeba bisibisi, hivi inaingia akilini kweli ubebe bisibisi kisha ucheze mpira?
“Huyo mwamuzi sijui amewaza nini, hata kama nilibeba hirizi kwani
kuna tatizo gani? Mbona wapo wengi tu wanabeba, hao kina Ngassa mbona
hamuwaandiki kuwa wanabeba hirizi!“Mi nashangaa sana nyie watu wa magazeti mnaniandika nimebeba bisibisi, hivi inaingia akilini kweli ubebe bisibisi kisha ucheze mpira?
“Mtu anaweza kubeba hirizi kwa kuwa ni sehemu ya kinga yake, kwani, mi najua hizi ni fitina tu za magazeti kwa kuwa nyie mnazipenda Yanga na Simba au hamkutaka tuifunge Yanga? Acheni hizo bana, mwambie na huyo mwandishi aliyeandika hiyo habari mi nitamshtaki,” alisema beki huyo.