A

A

Exclusive: Mike T aielezea Project ya wimbo wa 'JWTZ' waliofanya Jay Mo, Juma Nature na Profesa Jay na gwanda za kijeshi



Mwishoni mwa wiki iliyopita tulishuhudia project ya kipekee kuwahi kufanywa na wasanii wa Tanzania ambapo Juma Nature, Profesa Jay na Jay Mo walionekana kwenye kionjo cha video ya wimbo wa ‘JWTZ’ wakiwa wametupia gwanda za kijeshi huku wakiwa na kikosi halisi cha jeshi la wananchi Tanzania JWTZ.
Mike T, ambaye ni mmoja kati ya wahusika wakuu au organiser mkuu wa mradi huo akiwa na P Funk Majani, ameiambia tovuti ya Times Fm kuwa project hiyo hivi sasa inamilikiwa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
“Mmiliki wa ile project sasa hivi ni JWTZ wenyewe. Kwa sababu sisi tulipeleka idea, kwanza audio ilikuwa ni idea ambayo ni ya P-Funk kwa hiyo kwenye kui-visualise idea ni ya kwangu. Kwamba watu wameshaimba sawa, kwenye upande wa visual mimi nafanya nini. Kwa hiyo kila mtu alihusika kimpango wake.” Mike T ameiambia tovuti ya Times Fm.
Mnyalu ameeleza kuwa lengo la kuhakikisha ujumbe na historia ya JKT na JWTZ uwafikie vijana wengi ili wakiendelea kukua wawe wana ufahamu juu ya majeshi haya na vitu vingi vizuri yanayofanya.
Kupata nafasi ya kushuti na magwanda halisi ya kijeshi na kupewa sapoti ya kijeshi haikuwa kitu kirahisi kwa Mike T na wenzake hasa ukizingatia kuwa maeneo mengi ya jeshi hayarusiwi kupigwa picha.
“Mchakato kweli ni story ndefu, tumehangaika ila…yaani kifupi kwamba tunaweza kusema sasa hivi tumefungua njia tumejua njia yaani zote. Unajua zamani ile tumefanya wakati wengine tuko East Coast tulivyotumia kombati nini kilitokea. Yale makosa ndio yalinifunza mbele niweze kufanya kitu gani. Yaani ni story ndefu, tumekutana na mambo mengi na mpaka sasa hivi mambo mengi bado hayajatulia yaani upepo hapa katikati haujatulia. Ingawa project haijaisha lakini bado kuna mambo mengi.”
Ameeleza kuwa baada ya kupewa ruhusa ya kushuti alijikuta ameshuti vitu ambavyo haviruhusiwi na kwamba walipokuwa wanakagua walimtaka avitoe. Zoezi la ukaguzi wa video hiyo kwa mujibu wa Mike T lilirudiwa zaidi ya mara 9 huku vitu vingi vikiondolewa.
Hata hivyo utaratibu huo mgumu ulimfunza mengi Mike T ambaye anadai kuwa hivi sasa anafahamu nini cha kufanya  na hata naweza kuwaelekeza wasanii wengine utaratibu wa kupata nafasi kama hiyo ikiwa ni pamoja na waigizaji.

Project imeisha ila kuna mambo mengi sana ila tunaweza kusema kwamba tumefungua njia kwa watu wengine ambao watahitaji vitu kama vile wanawaweza wakatinitafuta tukakaa yaani nikawapa steps kwamba hiki kitu ABCD unaweza kufanya hivi. Kwa sababu kuna vitu ambavyo tulishuti ambavyo haviruhusiwi kuonekana. Kwa hiyo nayo iliniletea matatizo sana.
“Mwisho wa siku tuseme kutokana na yale makosa nimejua vitu vingi sana. Kwa hiyo mtu mwingine anaetaka kuja kufanya movie kutumia nini zile then nitampa utaratibu nini kinafanyika huko. Ukiangalia wenzetu huko Marekani wanatumia kombati wanafanya nini. Ilikuwa tatizo ni kwetu tu. Sio kwamba wanakataza lakini utaratibu tulikuwa tunatumia ambao sio mwanzoni.” Mike T amefafanua.