Siku
ya Jumamosi tarehe 22 Februari 2014 kilifanyika kikao baina ya Balozi
wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Peter Kallaghe pamoja na wawakilishi
wa Watanzania kutoka vitongoji vya London na maeneo mengine nchini
Uingereza.
Kikao hicho kilijadili haja ya kuandaa Mkutano wa Diaspora
nchini Uingereza mwaka huu 2014. Katika majadiliano ilisisitizwa
umuhimu wa kuwa na mikutano ya Diaspora hasa kwa malengo makuu
yafuatayo: • Kuwaleta karibu watanzania waishio maeneo mbalimbali nchini
Uingereza. • Kuwaweka karibu Watanzania na Serikali yao •
Kuwatangazia
Watanzania fursa zilizopo nyumbani katika sekta za maendeleo. Baada ya
majadiliano kikao kiliona haja ya kuandaa kamati ya muda (Tanzania UK
Diaspora Task Force) itakayosimamia mchakato wa maandalizi ya Mkutano wa
Diaspora mwaka huu 2014. Kamati hiyo itakuwa chini ya Uenyekiti wa Bi
Mariam Kilumanga akisaidiwa na Bw. Cleopa John katika nafasi ya Katibu.
Aidha Bi Maxine Brown atashughulikia mawasiliano kati ya kamati na
watanzania waishio nchini Uingereza kuelekea mkutano huo. Orodha ya
wajumbe wengine wa kamati hiyo itawasilishwa baadae.
Kamati hii itafanya
kazi kwa karibu na ofisi yetu ya Ubalozi kufanikisha Mkutano wa
Diaspora 2014. Kamati inaomba watanzania waishio Uingereza waupe uongozi
wa kamati ushirikiano katika kufikia lengo hili ambalo hatimaye ni kwa
manufaa ya watanzania wote na maendeleo ya nchi yetu.
Ahsanteni.
Tanzania-UK Diaspora Task
Force
Ahsanteni.
Tanzania-UK Diaspora Task
Force
No comments:
Post a Comment
Toa maoni yako lakini angalia kuchafua hali ya hewa na usimuumize mwenzako