A

A

Tamko la Mamlaka Ya Mapato Tanzania TRA Kwa Wafanyabiashara Wote kuhusiana na Mashine za EFD na Migomo inayoendelea

 
ISO 9001: 2008 CERTIFIED

PUBLIC NOTICE

Tanzania Revenue Authority would like to inform the general public that the ongoing shop closures is uncalled for and is highly regretted.
Let it be known that the issue of EFDs was passed by the Parliament of the United Republic of Tanzania in 2010.
This was followed by the official position of the President of the United Republic of Tanzania in his end of month Speech in March 2011 just before the commencement of phase 1 for VAT registered traders.
The Vice President of the United Republic of Tanzania Dr. Mohammed Gharib Bilal further reaffirmed this Position on 8th November 2013.
The Prime Minister Hon. Mizengo Peter Pinda also wound the Parliamentary Session in December 2013 by cementing the government’s position on the EFDs.
On 29th of January 2014, The Minister of Finance Hon Saada Mkuya Salum, further gave a statement during the press conference on the government’s position giving assurance on the determination to enforce the requirements of law. This was one among the many interventions the Ministry has stated the position to the business community and the General Public.
Tanzania Revenue Authority has done the same ever since phase 1 started in 2011 and has continued doing so throughout the second phase awareness until the beginning of the implementation.
Where operational issues arose they have been resolved and will continue to be resolved to the satisfaction of all parties.
TRA would therefore like to inform the business community that those forcing or persuading others to close shops should refrain from doing so as they are breaking the law by creating chaos unnecessarily. We have also regrettably noted that some of the businesses being forced or persuaded to close are not part of phase 2 implementation of EFD while those who decide to close on their own should do so on their own will and not otherwise. We are also receiving calls and requests for protection from those who do not wish to close shop but only do so because they are being threatened and intimidated.
Let it be known that those who are masterminding this unlawful move will be dealt with by the relevant arms of law while those who are being harassed should inform us through the following numbers 0786 800000, 0713800333 and 0800 110016 or by email: info@tra.go.tz

TOGETHER WE BUILD OUR NATION


ISSUED BY THE ACTING COMMISSINER GENERAL

 
ISO 9001: 2008 CERTIFIED

TAARIFA KWA UMMA

Mamalaka ya Mapato Tanzania inapenda kuufahamisha umma wa Watanzania na wafanyabiashara kwa ujumla Kuwa inasikitishwa  na mgomo wa wafanyabishara kwa kufunga maduka maeneo mbali mbali nchini.
Ifahamike kuwa Matumizi ya mashine ya EFD ni jambo la kisheria  na lilipitishwa na bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2011.
Pamoja na sheria kupitishwa, viongozi wakuu wa nchi walikwisha litolea tamko kwa nyakati tofauti kwa kuanzia na Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete katika hotuba yake ya kufunga mwezi wa Machi 2011.
Pia Makamu wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Mohammed Gharib Billal alikazia jambo hili tarehe 8 Mwezi November mwaka 2013.
Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Mhe. Mizengo Peter Pinda alilitolea tamko pia Mwezi Desemba 2013  wakati akiahirisha Bunge kwa kusisitiza msimamo wa serikali kwa utekelezaji wa kisheria wa matumizi wa mashine za EFD.
Tarehe 29 Janauri 2014, Waziri wa Fedha Mhe Saada Mkuya Salum aliweka bayana msimamo wa Serikali kwa kusisitiza kuwa Matumizi ya mashine za EFD ni swala la kisheria na litaendelea kutekelezwa kwa mujibu wa sheria akisisitiza kuwa muda wa mwisho wa nyongeza kwa wafanyabishara kununua mashine ilikuwa ni Tarehe 31 Januari 2014 baada ya kuongeza muda mara tatu kwa nyakati tofuati.
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) pia kwa nyakati tofauti na maeneo  tofuati imelitolea tamko jambo hili na itaendelea kufanya hivyo.
Kwa masuala ya kiutendaji yaliyolalamikiwa yamefanyiwa kazi na yanaendelea   kufanyiwa kazi ikiwemo utoaji wa Elimu kwa umma.
Mamlaka ya Mapato Tanzania  inapenda kuwafahamisha wafanyabiashara na umma kwa ujumla kuwa watu wanaolazimisha wafanyabishara wenzao kufunga maduka kwa kuwatishia na  kuwashurutisha wanavunja sheria kwa kusababisha uvunjifu wa amani nchini na hivyo mkono wa sheria utawafikia. Pia imefahamika kuwa baadhi ya watu wanaoshurutishwa kufunga biashara sio walengwa bali hutumika kuhalalisha azma ya wale wenye nia mbaya
TRA imekuwa ikipokea taarifa na maombi kutoka kwa baadhi ya wafanyabishara na wananchi wema wakiomba ulinzi ili wafungue maduka yao na kufanya biashara maana ndio ajira yao na mahali pakujipatia riziki ya kila siku.
Ifahamike kwamba wale wote wanaoshinikiza na kulazimisha wenzao kugoma wanavunja sheria kwa kuwalazimishwa wafanyabiashara kugomea agizo halali la kisheria hivyo kwa wale wote wanaotishiwa au kushurutiswa watoe taarifa kwa  kupiga simu namba zifuatazo 0786 800 000, 0713 800333, 0800 110016 au barua pepe info@tra.go.tz

“PAMOJA TUNAJENGA TAIFA LETU”

IMETOLEWA NA KAIMU KAMISHNA MKUU
MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA




No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako lakini angalia kuchafua hali ya hewa na usimuumize mwenzako