A

A

Baada ya Kutuma Man United,Mata akabidhiwa Jezi Adimu hii hapa


Mshambuliaji mpya wa Manchester United, aliyejiunga na wekundu hao akitokea Chelsea, Juan Mata, akionyesha Jezi yake namba 8, aliyokabidhiwa mara baada ya kumwaga wino katika chama lake jipya hilo.
**********************************
*MOYES AANZA KUCHONGA NGENGA
Siku chache tu baada ya kumnasa mshambuaji hatari, Kocha wa Manchester United, David Moyes sasa ameanza kuchonga na kujigamba kuwa anauhakika wa kurudisha matumaini kwa timu yake katika mechi zake zilizobaki baada ya kumsajiri mshambulizi huyo kwa dau la Pauni milioni 37 ambazo ni zaidi ya Sh. bilioni 70 za kitanzania.
Aidha Moyes aliongeza kwa kusema kuwa anatarajia kuendelea kufanya usajiri mkubwa na wa nguvu, siku zijazo kwa lengo la kuijenga timu itakayokuwa ya ushindani.
''Sitarajii kusajiri mchezaji mwingine katika kipindi hiki cha dirisha dogo bali najiandaa kukiimarisha kikosi changu nilichonacho kwanza,
Kwa ujio wa Mata kwangu ni faraja kubwa kwa kujiunga katika wakati huu muafaka''. alisema Moyes

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako lakini angalia kuchafua hali ya hewa na usimuumize mwenzako