A

A

Askari wa usalama barabarani afariki papo hapo kwa kugongwa na gari akiwa kazini

MNAMO tarehe 05.01.2014 huko eneo la Mbeya One, kata ya Isongole tarafa ya Ukukwe, barabra ya Mbeya/ Tukuyu wilayani Rungwe mkoani Mbeya, Askari EX WP 1601 S/SGT BENADETHA, (52), wa kikosi cha usalama barabarani akiwa kazini, aligongwa na gari T.613 BUMaina ya TOYOTA CARINA lililokuwa likiendeshwa na dereva ERNEST S/O MATHAYO NDOA, (35), mkazi wa Kyela na kusababisha kifo cha askari huyo papo hapo.


Taarifa ya jeshi la polisi imesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi. Dreva amekamatwa na gari lipo katika kituo cha polisi Tukuyu.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya AHMED. Z. MSANGI ametoa wito kwa madereva kuwa makini wanapotumia vyombo vya moto kwa kufuata sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako lakini angalia kuchafua hali ya hewa na usimuumize mwenzako