A

A

Buhari:Ni ushindi wa kidemokrasi Nigeria

Mshindi wa uchaguzi wa urais nchini Nigeria Muhammadu Buhari anasema kuwa ushindi wake unamaanisha kuwa taifa hilo linafuata mfumo wa kidemokrasi.
Buhari alimshinda mpinzani wake Goodluck Jonathan,kwa kura millioni 2 idadi ambayo wachanganuzi
wanasema kuwa itazuia harakati zozote za kuanzisha kesi.
Ni mara ya kwanza kwa rais wa taifa hilo kushindwa katika uchaguzi.
Bwana Buhari ,kiongozi wa zamani wa kijeshi alichukua mamlaka mnamo mwaka 1980 kupitia mapinduzi.
Hatahivyo alifanya kampeni za kidemokrasia kwa lengo la kutaka kusafisha siasa katika taifa hilo lenye idadi kubwa ya watu barani Afrika.
Katika hatua ya kidemokrasia,rais anayeondoka Goodluck Jonathan alimpigia simu Buhari kukubali ushindi na vilevile kutoa taarifa akiwataka wafuasi wake kukubali matokeo.
BBC

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako lakini angalia kuchafua hali ya hewa na usimuumize mwenzako