Stori: Waandishi Wetu/Risasi Mchanganyiko
Hakika wikiendi iliyopita
ilikuwa ni shangwe tupu, lakini kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia
leseni ya Chadema, Zitto Zuber Kabwe ilikuwa ya machungu pale
alipojikuta akimwaga chozi ukumbini.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia leseni ya Chadema, Zitto Zuber Kabwe akiwa na Christian Bela.
Mpango
mzima ulioshuhudiwa na paparazi wetu ulijiri kwenye Ukumbi wa Mango
Garden, Kinondoni jijini Dar ambapo Bendi ya Malaika, chini ya Christian
Bella ilikuwa ikishusha burudani ya kufa mtu.
Wakati
Mbunge wa Jimbo la Sikonge kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Said
Nkumba alitesa kwenye jukwaa la Msondo Ngoma pale TTC Chang’ombe,
Temeke, Zitto alifunika vibaya Mango Garden, Kinondoni, kwani alikuwa
zaidi ya shabiki, pedeshee na mwimbaji.
Katika
muda ambao watoto wa mjini husema ni usiku mnene, Zitto ambaye yupo
katika mgogoro na chama chake, alipanda jukwaani wakati prezidaa wa
Malaika Band, Christian Bella ‘Obama’ akiimba wimbo wake mpya wa ‘Nani
Kama Mama’ ambapo mheshimiwa huyo alichotwa na hisia za kibao hicho hadi
kujikuta akimwaga machozi kwa kumbukumbu ya msiba wa mama yake mzazi
uliotokea mwaka jana (Shida Salum, alifariki Juni 1, 2014 jijini Dar es
Salaam).
Mh. Zitto Kabwe akiteta jambo na wanamuziki wa Bendi ya Malaika.
“Lilikuwa
ni tukio la kushangaza kwa mheshimiwa, maana alipanda stejini kisha
akajiunga na waimbaji, akachukua gitaa na kuanza kucharaza kana kwamba
alifanya nao mazoezi,” alisema shabiki mmoja ukumbini hapo,
Hata
hivyo, baadaye mwanasiasa huyo kijana kipenzi cha wengi, aliimarika na
kuendelea kuuimba wimbo huo huku akiserebuka kwa kwenda mbele.
Baada ya kuona hivyo,
mashabiki walimiminika jukwaani kupiga naye picha kwa muda wa takriban
dakika 20, ambapo mbunge huyo alithibitisha kuwa ni mtu wa watu kwani
shughuli zote zilisimama kwa muda ukumbini humo.
Katika
hali hiyo, mapedeshee, ambao hung’ara katika kumbi kwa kutunza waimbaji
na wanenguaji, walizimwa ngebe zao kwani Zitto alifunika kwa kutoa
‘mshiko’ wa kufa mtu.
Ilifahamika kwamba, Bella
peke yake alipokea zaidi ya noti 50 za elfu kumi-kumi za Kitanzania
kutoka kwa Zitto huku nyingine zikiwa ni dola za Kimarekani.
Wakipiga picha ya pamoja.
Hata
hivyo, katika hali nyingine, baadhi ya watu walihoji usalama wa Zitto
kuwa ni sawa na sifuri katika kipindi hiki ambacho bado sakata la kashfa
ya uchotwaji wa mabilioni kwenye Akaunti ya Escrow ya Tegeta
linaendelea kushika kasi na vigogo kufikishwa mahakamani.
Watu
hao walisema kwa namna Zitto alivyoingia ukumbini hapo na kujichanganya
na mashabiki, ni rahisi kwa mtu mwenye nia mbaya kuweza kumdhuru, hasa
watu wa Escrow ambao wana mapesa yanayoweza kuwashawishi kumfanya
lolote.
“Watu
wanatetemeshwa na hili skendo, leo wakimuona Zitto hapa kajiachia namna
hii, watakumbuka jinsi alivyosimama kidete bungeni kutaka waliohusika
wawajibishwe na fedha zirudishwe, unadhani nani hajui utamu wa fedha,”
alisikika shabiki mmoja akisema.
Zitto alitafutwa kupitia simu yake ya mkononi ili kupata maoni yake juu ya usalama wake, lakini iliita bila kupokelewa.
No comments:
Post a Comment
Toa maoni yako lakini angalia kuchafua hali ya hewa na usimuumize mwenzako