A

A

UDOM inauarifu umma kuwa wafuatao si waajiriwa wake

TAARIFA KWA UMMA

 BWANA CHRISANTUS LUCAS MILANZI

Bwana Chrisantus Lucas Milanzi, mzaliwa wa Masasi Mtwara, ambaye picha yake inaonekana hapo juu, si mwajiriwa wa Chuo Kikuu cha Dodoma.

Chuo hakihusiki na muamala wowote unaofanywa na mhusika kwa niaba ya Chuo. Wananchi wenye malalamiko kuhusiana na miamala iliyofanywa au inayofanywa na muhusika kwa niaba ya Chuo wayafikishe kwenye vyombo vya dola kwa hatua za kisheria.

Wananchi wanaombwa kuzingatia kwamba Chuo Kikuu cha Dodoma kina taratibu za kuendesha shughuli zake kwa mujibu wa sheria.
Bw. Tito Ivan William

Chuo Kikuu cha Dodoma kinapenda kuutaarifu umma kuwa Bwana Tito Ivan William, mzaliwa wa Kijiji cha Mtumba - Manispaa ya Dodoma, ambaye picha yake inaonekana hapo juu, sio mwajiriwa wa Chuo Kikuu cha Dodoma kuanzia tarehe 31 Januari 2014.

Chuo Kikuu cha Dodoma hakitahusika na makubaliano yoyote yatakayofanywa na mhusika kwa niaba yake. Malalamiko yoyote (kama yatakuwepo) kuhusiana na mhusika, yapelekwe kwenye vyombo vya dola kwa hatua za kisheria.

Tunatanguliza Shukrani kwa Ushirikiano

IMETOLEWA NA OFISI YA UHUSIANO – CHUO KIKUU CHA DODOMA

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako lakini angalia kuchafua hali ya hewa na usimuumize mwenzako