A

A

TASWIRA,IRINGA MJINI JANA ILITIKISIKA,COMRADE MWIGULU NCHEMBA AACHA GUMZO

ABaada ya Kuingia Iringa Mjini,Mh:Mwigulu Nchemba akaamua kuingia Mtaani kutembelea Matawi ya chama na Kuzungumza na Wananchi.Hapa Msafara wake ukiwa soko la Mitumba Iringa Mjini,Vijana wa CCM Iringa Mjini wakiwa mitaani Iringa Mjini.Chipukizi wa Chama Cha Mapindizi Iringa Mjini wakiwa tayari kwa Kumpokea Mgeni Rasmi Mh:Mwigulu Nchemba.Mh:mwigulu akipewa mapokezi na chipukizi wa Chama cha Mapinduzi Iringa Mjini.Msafara wa Naibu Katibu Mkuu CCM Bara Ukielekea Viwanja vya Mkutano.Naibu Katibu Mkuu CCM Bara Mwigulu Nchemba akiingia Viwanja vya Mwembetogwa Iringa Mjini tayari kwa Kumsimika Kamanda wa UVCCM Ndugu Salim Asas.Vijana wa Chama cha Mapinduzi Iringa wakifikisha Ujumbe wao kwa Watanzania.Kiongozi wa Madereva Bodaboda na Bajaji Iringa Mjini akisalimiana na Mh:mwigulu Nchemba na Kupongezwa namna anavyosimamia Uendeshaji wa Bajaji na Bodaboda Iringa Mjini.Naibu Katibu Mkuu CCM Bara akielekea Kupandwa Jukwaani tayari kwa Kuzungumza na Wakazi wa Iringa Mjini.
 Comrade Mwigulu Nchemba akisalimiana na Wananchi.Mh:Mwigulu Nchemba akisisitiza Umoja ndani ya Chama na Jumuia zake.Sehemu ya Mamia ya Wananchi waliofurika Uwanja wa Mwembetogwa kushuhudia zoezi la Kuapishwa kwa Kamanda wa UVCCM Ndugu.Salim Asas.Mwigulu Nchemba akzungumza na Wananchi waliofurika uwanja wa Mwembetogwa namna  Wizara yake ilivyoanza mikakati ya Kuhakikisha Fedha za Watanzania zinatumika ipasavyo kwenye kazi za Maendeleo,Pia lisisitiza Kubana matumizi serikalini ndio kipaumbele cha Ofisi yake kwa wakati wote wa Utendaji kazi wake.Naibu Katibu Mkuu CCM Bara Comrade Mwigulu Nchemba akipata picha ya pamoja na Kamanda wa UVCCM Iringa Ndugu.Salim Asas.Katikati ni Mwenyekiti wa CCM MKoa wa Iringa Bi.Jesca Mtasavangu.Baadae Mh:Mwigulu Nchemba alitawazwa kuwa Chief wa Kihehe kama Unavyomuona ndani ya Vazi la Kichifu.
Mh:Mwigulu Nchemba akiwaaga Wananchi waliofika kwenye Shughuli ya Kusimikwa kwa Kamanda wa UVCCM Iringa.
Picha/Maelezo na Festo Sanga.

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako lakini angalia kuchafua hali ya hewa na usimuumize mwenzako