A

A

KAMATI YA UONGOZI YA BUNGE MAALUM YAFANYA KIKAO CHAKE CHA KWANZA LEO ...


 Mwenyekiti wa Bunge Maalum Mhe. Samuel Sitta akiongoza kikao cha kwanza cha kamati ya Uongozi baada ya kuundwa leo. Kamati hiyo inayoundwa na wenyeviti wa Kamati za Bunge Maalum wote 12  pamoja na mambo mengine inajukumu la kaundaa ratiba ya Bunge Maalum. Kushoto kwake ni Katibu wa Bunge Maalum Yahya Khamis Hamad na aliyekaa kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum Mhe. Samia Suluhu Hassan.
 Mhe. Sitta akiendelea kuongoza Kikao cha Kamati ya Uongozi
 Naibu Katibu wa Bunge Maalum Dkt. Thomas Kashililah akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa kamati ya Bunge Maalum kuhusu uwezo wa kutumika kupigia kura vifaa vya kielekroniki vilivyofungwa katika ukumbi wa Bunge wakati kamati hiyo ilipokutana jana.
 Mjumbe wa Kamati ya Uongozi Mhe. Anna Abdalah akifafanua jambo wakati wa kikao cha kamati hiyo.
 Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Bunge Maalum wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wakati wa kikao hicho.
Sehemu ya wajumbe...Picha na Owen Mwandumbya 
Na Magreth Kinabo,  MaelezoDodoma   
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba,Mhe. Samwel Sitta leo, ametangaza majina ya wenyeviti na makamu wenyeviti wa Kamati za bunge hilo.

Majina hayo yametangazwa na Mwenyekiti huyo  baada ya uchaguzi wa viiongozi hao uliofanyika (jana) Machi 24 , mwaka  2014 mjini  Dodoma .

Mwenyekiti huyo aliyataja majina hayo  katika  Kamati  ya Uandishi Mwenyekiti Andrew Chenge, Makamu wake ni Mgeni Hassan Juma. Kamati ya Kanuni Mwenyekiti ni Pandu Ameri Kificho, Makamu wake ni Dkt. Susan Kolimba. Kamati Na. 1 Mwenyekiti ni  Ummy Ally Mwalimu, na Makamu wake ni Prof. Makame  Mbalawa.

Wengine waliochaguliwa  katika Kamati Na. 2 Mwenyekiti ni Shamsi Vuai Nahodha, Makamu wake ni Shamsa Mwangunga.Kamati Na. 3 Mwenyekiti  ni  Dkt. Francis Michael, Makamu wake ni Fatma MussaJuma.

Mhe. Sitta alisema waliochaguliwa katika Kamati Na. 4 Mwenyekiti ni  Christopher  Ole-Sendeka, Makamu wake ni  Dkt. Sira Ubwa Mamboya, Kamati Na. 5 Mwenyekiti ni  Hamad Rashid Mohamed Makamu wake ni  Assumpter  Mshama.

          Viongozi waliochaguliwa katika Kamati Na. 6 Mwenyekiti Stephen Wassira na Makamu wake ni Dkt. Maua  Daftari.Kamati Na. 7  Mwenyekiti  Brig. Hassan Ngwilizi  ,Makamu wake  Waride   BakariJabu.Kamati Na. 8 Mwenyekiti  ni Job Ndugai,Makamu wake ni Biubwa Yahya   Othman.

Kamati Na. 9 Mwenyekiti ni Kidawa Hamidi Saleh,Makamu wake Wiliam  Ngeleja,Kamati Na. 10 Mwenyekiti ni Anna  Abdallah, Makamu wake ni   Salmin Awadh Salmin.Kamati Na. 11 Mwenyekiti ni Anne  Malecela, Makamu wake  Hamad  Masauni na Kamati Na. 12 Mwenyekiti  Paul Kimiti na Makamu wake ni  Thuwaybah E. Kisasi.

Wakati huohuo , Sitta  alitangaza wajumbe wa Kamati ya  Uongozi ya Bunge Maalum la Katiba, ambao  ni wenyekiti na makamu wenyeviti wa kamati hizo wakiwemo wajumbe wengine watano aliowateua.

 Wajumbe hao walioteuliwa na Sitta kuingia katika kamati hiyo ni Fakharia Khamisi Shomari, Mary Chatanda, Profesa Ibrahim Lipumba, Amon Mpanju na Hamad Abuu Juma.

 Hata hivyo pamoja na majina hayo kutangazwa Profesa Lipumba alisimama na katika nafasi hiyo .